1. Wezesha usasishaji wa kiotomatiki wa programu

Mojawapo ya mambo muhimu zaidi ya kuweka rilei yako salama ni kusakinisha masasisho ya usalama kwa wakati unaofaa na kiotomatiki ili usiweze kusahau kuihusu. Fuata maelekezo ili kuwezesha usasishaji wa programu ya kiotomatiki kwenye mfumo wako wa uendeshaji.

2. Sanidi hazina ya mradi wa Tor

Kusanidi hifadhi ya mradi wa Tor kwa Fedora kimsingi inajumuisha kusanidi /etc/yum.repos.d/Tor.repo na maudhui yafuatayo:

[tor]
name=Tor for Fedora $releasever - $basearch
baseurl=https://rpm.torproject.org/fedora/$releasever/$basearch
enabled=1
gpgcheck=1
gpgkey=https://rpm.torproject.org/fedora/public_gpg.key
cost=100

Habari zaidi juu yake inaweza kupatikana hapa.

3. Usakinishaji wa kifurushi

Sakinisha kifurushi cha tor:

# dnf install tor

4. Faili ya Usanidi

Weka faili ya usanidi /etc/tor/torrc mahali pake:

Jina la utani    myNiceRelay  # Badilisha "myNiceRelay" iwe kitu unachokipenda
ContactInfo your@e-mail  # Andika barua pepe yako ukiwa unafahamu kuwa itachapishwa
ORPort      443          # Unaweza kutumia bandari tofauti ikiwa utataka
ExitRelay   0
SocksPort   0

5. Anzisha huduma

# systemctl enable --now tor

6. Maelezo ya mwisho

Ikiwa unapata shida kusanidi rilei yako tazama sehemu ya msaada wetu. Ikiwa rilei yako inaendeshwa sasa angalia maelezo ya baada ya kusakinisha.